
gari aina ya Toyota Canter zinazobeba abiria huko Zanzibar inayofahamika zaidi kwa jina la chai maharage,ikiwa katika mingo zake za kila siku katika moja ya barabara za huko Zenj.

gari aina ya Toyota Canter zinazobeba abiria huko Zanzibar inayofahamika zaidi kwa jina la chai maharage,ikiwa katika mingo zake za kila siku katika moja ya barabara za huko Zenj.
NDUGU WADAU WATEMBELEAJI WA BLOG YETU HII,KUTOKANA NA SABABU ZILIZO NJE YA UWEZO WANGU KATIKA KIJIJI HIKI,AMBAZO ZINANIFANYA NISHINDWE KUENDELEZA LIBENEKE KATIKA BLOG YETU HII NA KUNIFANYA NIRUDI TENA KWENYE BLOG YETU YA ZAMANI (othmanmichuzi.blogspot.com) AMBAYO NILIISIMAMISHA KWA MUDA KWA KUWA ILIKUWA KWENYE MATENGEZO NA SASA MATENGENEZO YAKE YAMESHAFIKIA TAMATI NA LIBENEKE LINAENDELEA KAMA KAWAIDA,HIVYO SINA BUDI KUWAREJESHA TENA KULE KWA ZAMANI KWANI SINA JINSI YA KUFANYA ZAIDI YA KUWARUDISHA KULE KWA ZAMANI ,HIVYO NAOMBENI RADHI SANA KWA USUMBUFU HUU ULIOJITOKEZA WADAU WANGU WATUKUFU.KWA HIYO KUANZIA LEO HII NA SIKU ZIENDELEZO HUKO MBELE KIJIJI HIKI MKIPENDACHO KITASIMAMA NA BADALA YAKE KIJIJI CHA ZAMANI KITACHUKUA NAFASI YAKE KAMA ILIVYOKUWA HAPO AWALI,HIVYO NAWAOMBENI WOOTE MNAOTEMBELEA KIJIJI HIKI KUENDELEA KUTEMBELEA KIJIJI CHETU KILE CHA ZAMANI YAANI NIKIMAANISHA othmanmichuzi.blogspot.com,NAWASHUKURUNI SANA TENA SANA KWA MCHAGO WENU NA NAOMBA TUENDELEE KUWA PAMOJA KAMA ILIVYOKUWA KATIKA MTAA HUU.
AHSANTENI SANA
-MICHUZIJR

“SATOLICIOUs”
By MUSTAFA HASSANALI
In
ROCK CITY MWANZA
Featuring:
Curtain Raiser by Mwanza Based Designer
CHRIS GEORGE
TOP models from DAR and MWANZA
DATE: 4 APRIL 2009
VENUE: NEW MWANZA HOTEL
TIME: 8.00P.M
DRESS CODE: STYLISH
TICKETS: VIP 20,000P/P
Normal 10,000P/P
Tickets Available at NEW MWANZA HOTEL from 1 APRIL
For More Information CALL/TEXT 0784303880
Or EMAIL: info@mustafahassanali.net
SPONSORED BY:
ZAIN….Our Wonderful World,
COCA-COLA
and
NYANZA ROAD WORKS LTD
NOTE: Thank you for your ALWAYS support in DISSEMINATION of Information. Stay in touch +255784303880
Hii ni staili mpya ya kupaki magari makubwa kwa pembezoni mwa barabara,hii kitu nimeinyaka jana mchana katika barabara ya Bagamoyo rodi.chini ni jinsi ionekanavyo kwa nyuma.
hili ni moja ya magali ya kujifunzia udereva kwa daraja la leseni aina C,ambapo mafunzo yapatikanayo ndani ya ndinga hii ni pamoja na kuweza kuendesha magari yabebayo abiria na mengine.sasa swali langu ni kwa madereva waliowengi wanaoendesha magari yabebayo abiria,je madereva hao ni kweli wamepitia huku???
Leo nilipata wasaha mwingine wa kukutana na washkaji wa kijiji cha jirani kinachokwenda kwa jina hili bofya hapa,nilipogongana nao pale maeneo ya kijitonyama katika kiota cha Chaga Bite,Toka (shoto) ni Charles,Mariam pamoja na Broo Young (jina lake la kwanza limenitoka sasa hivi,ngojeni nikumbuke halafu nitawatajia) na mwisho kabisa ni nanihii wa nanihii ya nanihii.
maana nipokutana na madogo hawa nilifikiria mengi sana kuhusiana na makuzi niliyokuwa nimepitia enzi hizooooo

barabara ya Kilwa rodi a.k.a Mbagala rodi inavyoonekana leo hii,siku hizi kutoka Mbagala hadi mjini ni dakika kadhaa tu tofwauti na siku za awali ambapo ilikuwa ukitoka Mbagala saa 12 asubuhi basi utafika mjini saa 3 asubuhi.hii hali inapendeza kwa kweli.
picha na Mroki wa Mroki
Kamanda wa Trafiki Dar es salaam,Afande Mohamed Mpinga (shoto) na Naibu Mkurugenzi wa upelelezi wa makosa ya jinai Afande Peter Kivuyo (kati) na Mbunge wa Bariadi Mashariki Mh. Andrew Chenge wakielekea sehemu iliyotokea ajali ambapo gari alilokuwa akiendesha Mh. Chenge liligongana na Bajaji jana alfajiri na kusababisha vifo vya abiria wawili wa Bajaji hiyo.
Gari alilokuwa akiliendesha Mh.Andrew Chenge,likiwa kituo cha Polisi Cha Osterbay.
Mwanza, Tanzania Second Largest City, The economic Hub of the Lake region will For the First Time be dazzled by glitz glamour and gallantry synonymous with the creation of Renowned Designer Mustafa Hassanali Who shall be showcasing his Art on 4 April 2009 at the NEW MWANZA HOTEL from 8.00P.M
Top Models from Dar es Salaam and Mwanza Shall not Only Parade Mustafa Hassanali Designs but also that of Mwanza OWN CHRIS DESIGNER… who shall be the Curtain Raiser.
Mustafa Says “Having done so many Shows in Dar es Salaam, Twice in Arusha and once in Zanzibar, it’s now the right time to launch my collection to the people Of Mwanza. It’s a step aimed at not only Promoting Fashion as a lifestyle trend in Tanzania but also Promoting Made in Tanzania Products”.
Entry to The show is slated at Tsh 20,000 for VIP tickets and 10,000Tsh only for Normal Seats
The SATOLICIOUS Fashion Show in Mwanza is Proudly Sponsored By ZAIN….Our Wonderful World, Coca-Cola and Nyanza Road Works.
Rais Jakaya Kikwete ameteua Wakuu wa Wilaya 15 , 7 wamestaafishwa na 54 wamehamishwa vituo, ili kuongeza chachu ya uwajibikaji katika kusimamia na kuratibu mipango mbalimbali ya maendeleo na uchumi ili kutimiza malengo ya serikali.
Kwa mujibu wa taarifa toka Ofisi ya Waziri Mkuu, Ma-DC wawili wamepangiwa kazi zingine na wawili wengine wamepangwa kufanya kazi katika jumuiya za chama tawala – CCM.
Walioteuliwa kwa mara ya kwanza ni Ms Mercy Sila (Arumeru – Arusha), Mr Norman Sigalla (Hai – Kilimanjaro), Col Issa Njiku (Misenyi – Kagera), Ms Angelina Mabula (Karagwe – Kagera), Dr Rehema Nchimbi (Newala – Mtwara), Francis Isaac (Mbulu – Manyara), Lt Col Benedict K Kitenga (Rorya – Mara) na Lt Col Cosmas Kayombo (Mbarali – Mbeya).
Wengine ni Christopher Ryoba Kangoye (Kwimba – Mwanza), Queen Mashinga Mulozi (Ukerewe – Mwanza), Fatuma Mwassa (Mvomero – Morogo), Fatma Ally (Nanyumbu – Mtwara), Juma Solomon Madaha (Tunduru – Ruvuma), Anatory Choya (Kishapu – Shinyanga) na Erasto Sima (Korogwe – Tanga).
Ma-DC waliostaafu ni Elias Marugu (Misenyi – Kagera), Deusdedit Mtambalike (Muleba – Kagera), David Holela (Babati – Manyara), Hawa Ngulume (Mbarali – Mbeya), Mashiba H Mashiba (Kyela – Mbeya), Col Peter Madaha (Nyamagana – Mwanza) na Gilbert Dololo (Kibaha – Pwani).
Ma-DC waliopangiwa kazi zingine ni Patrick Tsere aliyekuwa DC (Ilala – Dar es Salaam), na Doreen Kisamo (Uyui – Tabora). Mr Martin Shigela ambaye alikuwa DC (Lindi – Lindi) sasa ni Katibu Mkuu wa UVCCM ambapo Husna Mwilima (Hai – Kilimanjaro) sasa ni Katibu Mkuu wa UWT.
Waliobadilishwa vituo ni pamoja na Elias W. Lali kutoka Arusha – Arumeru kwenda Ngorongoro, Evans Balama toka Arusha – Arusha kwenda Ilala, Jowiko W Kasunga kutoka Arusha – Ngorongoro kwenda Monduli, Col Fabian I Massawe toka Dar es Salaam – Kinondoni kwenda Muleba, Abdallah A Kihato toka Dar es Salaam –Temeke kwenda Kyela.
Wengine ni Zainab Kwikwega toka Dodoma – Bahi kwenda Kasulu, Dr Ian J. Langiboli toka Dodoma – Chamwino kwenda Babati, Capt Seif A. Mpembenwe toka Dodoma – Kondoa kwenda Handeni, Halima Dendego toka Dodoma – Mpwapwa kwenda Kilosa, Lephy B Gembe toka Iringa – Makete hadi Chamwino na Elaston J. Mbwilo toka Iringa – Iringa kwenda Mtwara.
Wengine ni Darry I Rwegasira toka Iringa – Njombe kwenda Mpwapwa, Said M Mkumbo toka Kagera – Chato kwenda Temeke, Frank A Uhahula toka Kagera – Karagwe kwenda Tarime, Lt Col John Mzurikwao toka Kigoma – Kibondo kwenda Mpanda, Saidi Bwanamdogo toka Kigoma – Kasulu kwenda Kondoa, Raymond H Mushi toka Kilimanjaro – Rombo kwenda Arusha.
Wengine ni Jordan Rugimbana toka Kilimanjaro – Mwanga hadi Kinondoni, Rashid M Ndaile toka Lindi – Nachingwea kwenda Chunya, Anna Magowa toka Lindi – Liwale kwenda Hanang, Elias Goroi toka Manyara – Mbulu kwenda Nachingwea, Capt Geoffrey Ngatuni toka Manyara – Hanang kwenda Musoma.
Walohamishwa wengine ni Saveli Maketta toka Mara – Musoma hadi Namtumbo, Stanley Kolimba toka Mara – Tarime kwenda Uyui, Ms Miriam L Lugaila toka Mbeya – Rungwe hadi Misungwi, Halima Kihemba toka Mbeya – Mbozi kwenda Kibaha, Fatuma L Kimario toka Mbeya – Chunya kwenda Igunga.
Wengine ni Athuman H Mdoe toka Morogoro – Kilosa kwenda Mwanga, Hawa Ng’humbi toka Morogoro – Mvomero hadi Makete, Gishuli M Charles toka Mtwara – Mtwara kwenda Njombe, Jackson W Msome kutoka Mtwara – Newala kwenda Rungwe, Capt Assary Geofrey Msangi toka Mtwara – Nanyumbu kwenda Iringa.
Wengine ni Samwel Kamote toka Mwanza – Ilemela hadi Bukoba, Danhi Makanga toka Mwanza – Kwimba kwenda Kibondo, Magalula S Magalula toka Mwanza – Misungwi hadi Lindi, Paul Chiwile toka Mwanza – Ukerewe kwenda Liwale, Mathew K Nasei toka Mwanza – Magu kwenda Muheza, Lt Col Serenge M. Mrengo kutoka Pwani – Bagamoyo hadi Ilemela, Ali N Rufunga toka Pwani – Rufiji kwenda Manyoni.
Wengine ni Major Bahati Matala toka Rukwa – Sumbawanga kwenda Kahama, Thobias Mazanzala toka Rukwa – Mpanda kwenda Sumbawanga, Gabriel Kimolo toka Ruvuma – Namtumbo kwenda Mbozi, Peter Toima Kiroya toka Ruvuma – Tunduru kwenda Rombo, Amina Masenza toka Ruvuma – Mbinga kwenda Shinyanga.
Waliohamishwa vituo wengine ni Khadija R R Nyembo toka Shinyanga – Kishapu kwenda Chato, Col (rtd) Edmund Mjengwa toka Shinyanga – Shinyanga kwenda Mbinga, Magesa Mulongo toka Shinyanga – Bukombe kwenda Bagamoyo, Florence A Horombe toka Singida – Singida kwenda Bukombe, Pascal Mabiti toka Singida – Manyoni kwenda Singida, Cleophas Rugarabamu toka Tabora – Igunga kwenda Nyamagana.
Wengine ni Kassim Majaliwa Majaliwa toka Tabora – Urambo kwenda Rufiji, Lt Winfrid F Ligubi toka Tanga – Handeni kwenda Urambo, Elizabeth Mkwasa toka Tanga – Korogwe kwenda Bahi na Zainab Kondo toka Tanga – Muheza kwenda Magu.