Archive

Archive for December 24, 2011

Mahafali ya Saba ya Chuo kikuu cha Taifa SUZA yafanyika leo Zanzibar

December 24, 2011 Leave a comment
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,pia Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar SUZA,Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na wahitimu wa Mahafali ya Saba ya Chuo hicho (hawapo pichani) kabla ya kuwatunuku shahada zao katika mahafali hayo yaliyofanyika leo Viwanja vya Chuoni hapo Vuga Mjini Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,pia Mkuu wa Chuo kikuu cha Taifa SUZA Dk Ali Mohamed Shein,akimtunuku Shahada ya heshima ya chuo kikuu cha Taifa cha SUZA Rais Mstaafu wa
Zanzibar Dr Amani Abeid Karume,wakati wa mahafali ya 7 yaliyofanyika katika viwanja vya chuo Mnazi mmoja Mjini Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,pia Mkuu wa Chuo kikuu cha Taifa SUZA Dk Ali Mohamed Shein,akimkabidhi zawadi Said Salum Bakhresa,kwa mchango wakemkubwa kukisaidia
Chuo,wakati wa mahafali ya 7 yaliyofanyika katika viwanja vya chuo Mnazi mmoja Mjini Zanzibar.
Wajumbe wa Bodi ya Chuo cha SUZA,Simai Mohamed (kushoto)na Mfanya biashara maarufu Said Bakhresa na Dr Nariman Jidawi,walipompongeza kwa kupata zawadi kutokana na mchango wake mkubwa kwa SUZA,wakati wa mahafali ya 7 chuoni hapo.
Wahitimu wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar SUZA wakisubiri kutunukiwa Shahada zao na Mkuu wa Chuo hicho ambaye pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza La Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein katika Mahafali ya Saba ya Chuo hicho yaliyofanyika leo Viwanja vya Chuoni hapo Vuga Mjini Zanzibar.
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar SUZA na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza La Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein wa katikati waliokaa akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa SUZA pamoja na wahitimu wa Chuo ngazi ya Stashahada baada ya kuwatunuku Stashahada zao katika Mahafali ya Saba ya Chuo hicho yaliyofanyika leo Viwanja vya Chuoni hapo Vuga Mjini Zanzibar.picha na Ramadhan Othman IKULU ZANZIBAR.
Categories: Uncategorized

ZIARA YA MH. BENDERA , WILAYANI ULANGA , KUANGALIA UHARIBIFU WA MAZINGIRA KWENYE BONDE LA KILOMBERO

December 24, 2011 Leave a comment
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro,Mh. Joel Bendera akionesha mpaka kati ya Kijiji cha Igawa, Malinyi na Pori Tengefu la Bonde la Kilombero, ambapo wananchi wamevamia kwa kulima na kufanya malisho ya mifugo yao.
Diwani wa Kata ya Malinyi , Said Tira wa Chadema ( kulia) akieleza jambo kwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro,Mh. Joel Bendera ( kati) huku Diwani mwenzake wa CCM Kata ya Igawa,Severus Kamguna, akisikiliza kwa makini
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro,Mh. Joel Bendera, (mwenye miwani) akifuata nyayo za RPC Adolfina Chialo aliyeongoza mstari, kwenda kuangalia uharibifu wa Bonde la Kilombero.
Mifugo nayo ndani ya Pori Tengefu la Bonde la Kilombero
Makazi ya jamii ya wasukuma ndani ya Pori Tengefu, Bonde la Kilombero
Gari la Polisi , Wilaya ya Ulanga, likiwa limenasa kwenye tope , ndani ya mashamba yaliyolimwa katika Bonde la Kilombero.
Baadhi ya wananchi wa Kata ya Igawa, Tarafa ya Malinyi, wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Morogoro,Mh. Joel Bendera (hayupo pichani), wakati alipotoa amri ya kuzuia shunghuli za kilimo na ufugaji katika bonde la Kilombero.
Baadhi ya wakulima wa Wilaya ya Ulanga waliovamia bonde la Kilombero , wakirejea baada ya kupata maekelezo ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro,Mh. Joel Bendera ( hayupo pichani).
Baadhi ya wakulima na wafugaji wa jamii ya kisukuma, wakitoka mashambani ili kumsikiliza Mh. Bendera (hayupo pichani).
Sehemu ya Mashamba makubwa yaliyilimwa ndani ya Pori Tengefu katika Bonde la Kilombero, eneo la Maguba, Malinyi , Wilaya ya Ulanga.Picha na John Nditi.
Categories: Uncategorized

misaada mbalimbali yaendelea kupokelewa na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam kwa kuwasaidia waliofikwa na janga la mafuriko

December 24, 2011 Leave a comment
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Mh. Said Meck Sadiq (wa tatu kushoto) akipokea sehemu ya misaada iliyotolea na Umoja wa Masheikh na Wanazuoni wa Nchini Tanzania wenye jumla ya thamani ya sh. Milioni 12,kutoka kwa Katibu Mkuu wa Umoja huo,Sheikh Hamis Mataka (mwenye kanzu nyeusi) leo kwenye ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.Wengine pichani ni wajumbe wa Umoja huo wa Masheikh.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Masheikh na Wanazuoni Nchini,Sheikh Hamis Mataka (katikati) akisoma taarifa fupi ya misaada mbali mbali iliyotolewa na umoja huo kwa ajili ya waathirika wa janga la Mafuriko lililolikumba jiji la Dar es Salaam hivi karibuni wakati walipofika kwenye ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Mh. Said Meck Sadiq (wa pili kulia) leo kwa ajili ya kukabidhi msaada huo.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Mh. Said Meck Sadiq akitoa shukrani kwa wale woote waliofika ofisini kwake leo kwa lengo la kuwasilisha midaada mbalimbali kwa ajili wa waathirika wa Mafuriko yaliyotokea hivi karibu jijini Dar.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Mh. Said Meck Sadiq (kulia) akipokea Misaada ya vyakula kutoka kwa vijana wanaounda Muungano wa Mashirika ya Vijana nchini,Kushoto ni Kiongozi wa Muundano huo,Nyakia Ally na Katikati ni Mjumbe wa Muungano huo,Sostenes Mitti.
Kiongozi wa Muungano wa Mashirika ya Vijana nchini,Nyakia Ally (kushoto) akiongea na vyombo vya habari wakati wa kukabidhi sehemu ya misaada kwa ajili ya waathirika wa Mafuriko jijini Dar es Salaam wakati walipofika kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Mh. Said Meck Sadiq (kulia) kukabidhi misaada yao hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Mh. Said Meck Sadiq (kushoto) akisikiliza kwa makini taarifa ya Meneja Mauzo wa DarBrew LTD ambao ni Watengenezaji wa Kinywaji cha Chibuku,Urban Shayo wakati walipofika ofisini kwa Mkuu wa Mkoa kwa ajili ya kukabidhi Msaada wao kwa waathirika wa Mafuko.
Categories: Uncategorized
Follow

Get every new post delivered to your Inbox.